Karibuni kwenye Wabongomeet Blog

Jitafutie rafiki na mchumba hapa Wabongomeet.....


Kwa wale wote ambao watapenda kuweka picha pamoja na info zao, tafadhali tuma kwa kupitia email wabongomeetinfo@gmail.com Nakaribisha maswali pamoja na maoni yenu.







Wednesday, January 21, 2009

Akina dada mnazidi kukaribishwa.

Dada na wadogo zangu mnazidi kukaribishwa kwenye blog yenu kwa kujitafutia marafiki mbalimbali ulimwenguni kote. Ni jambo la kutia moyo Ms. U. Sirikwa aliponitumia ujumbe kuwa kakutana na rafikiye huko Tanzania kupitia blog hii. Hii inatia moyo ingawa ndo waanza ku-date.

Ninazidi kuhamasiha mtume ujumbe, na kwa wale wenye picha ni vizuri zaidi maana wengi wanapenda kuanza kwa kuangalia picha. Na mara nyingi mwenye picha anapata hits nyingi. Hivyo msisite kuitumia blog yenu vilivyo, nitumieni picha kwa kutumia email wabongomeet@gmail.com Profile zenu zitakuwa posted jinsi nyie mnavyopenda, nitaheshimu matakwa yenu kama nilivyofanya kwa members wengine hapa.

KARIBUNI
Da Joesphine.

Sunday, January 18, 2009

Ambaye Yuko Tayari Tuwasiliane.

JOEL FRANK.

Hi,
JE WEWE NI BINTI WA KIPARE? UNAKIJUA KIPARE? LETS CONNECT!!!!!

Naitwa Joe kwa sasa naishi na kufanya Kazi Kahama katika mgodi mmoja maarufu. Age yangu ni 29 years na elimu yangu ni degree. Mie ni Mpare lakini sikuwahi ishi upareni hivyo kipare sikijui but natamani sana kukijua mana ndio roots zangu. Kwa sababu hii na kwa sababu nyingine binafsi ndio maana nimejitokeza katika forum hii KUTAFUTA MPENZI/MCHUMBA WA KIPARE!!!!!!! Imekuwa bahati mbaya sijawahi kuwa na rafiki wa karibu wa kipare ambaye angenifaa. Naamini sehemu hii ni mahali mwafaka kupata mmoja. Wengi wetu hatujajua kuwa Technolojia imekuja kurahisisha maisha yetu hivyo tunadhani huwezi kudate kupitia internet. Kwangu mi naona ni uzamani huo mana njia yoyote ni sahihi ilimradi tu at the end of the day kuna maridhiano kati ya wawili.

Kama wewe ni binti wa kipare na unayejiamini katika maisha, una mwanga wa elimu, na unadhani una sifa zimfanyazo mwanamke wa kipare please nicheki kupitia joelamref1978@yahoo.com na utashangaa what life has in store for the two of us.

__________________________________





DAVID NGOIYA
Personal Particulars:
Profession: Land Surveyor

Date of Birth: July 1973

Nationality: Tanzania

Postal address:

P O Box 23231 DSM

Cell phone + 255 755 829398/ + 255784236682

Email:ngoiya007@yahoo.com


Saturday, January 17, 2009

Wabongo watafutao marafiki na wachumba.




Kwa mara nyingine, watanzania popote duniani mnapewa nafasi katika kutafuta marafiki na hata wachumba popote duniani. Ukijaribu kuangalia sites za wengine unakuta huduma hii inalipiwa. Sisi watanzania tunajijua linapokuja suala la uchumi, lakini hii isiwe sababu ya watu kushindwa ku-network na wengine duniani.

Blog hii bado changa, huwezi kulinganisha na wengine ambao walianza ku-blog mapema. Hata hivyo hali hii haiwezi kusababisha watu wakashindwa kuanza kutafuta marafiki na hata wachumba popote duniani.

Matusi hapa hayatavumiliwa hata kidogo. Watanzania kama watanzania tuna wajibu wa kulinda utamaduni wetu wa kuheshimiana. Kwa wale ambao watapenda kuweka picha zao hapa mnakaribishwa. Mnaweza kutuma hizo picha kwa kutumia baruapepe wabongomeetinfo@gmail.com

Mnakaribishwa wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote ili mradi tunatunziane heshima.

Admin-Wabongomeet.