Karibuni kwenye Wabongomeet Blog

Jitafutie rafiki na mchumba hapa Wabongomeet.....


Kwa wale wote ambao watapenda kuweka picha pamoja na info zao, tafadhali tuma kwa kupitia email wabongomeetinfo@gmail.com Nakaribisha maswali pamoja na maoni yenu.







Saturday, January 17, 2009

Wabongo watafutao marafiki na wachumba.




Kwa mara nyingine, watanzania popote duniani mnapewa nafasi katika kutafuta marafiki na hata wachumba popote duniani. Ukijaribu kuangalia sites za wengine unakuta huduma hii inalipiwa. Sisi watanzania tunajijua linapokuja suala la uchumi, lakini hii isiwe sababu ya watu kushindwa ku-network na wengine duniani.

Blog hii bado changa, huwezi kulinganisha na wengine ambao walianza ku-blog mapema. Hata hivyo hali hii haiwezi kusababisha watu wakashindwa kuanza kutafuta marafiki na hata wachumba popote duniani.

Matusi hapa hayatavumiliwa hata kidogo. Watanzania kama watanzania tuna wajibu wa kulinda utamaduni wetu wa kuheshimiana. Kwa wale ambao watapenda kuweka picha zao hapa mnakaribishwa. Mnaweza kutuma hizo picha kwa kutumia baruapepe wabongomeetinfo@gmail.com

Mnakaribishwa wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote ili mradi tunatunziane heshima.

Admin-Wabongomeet.

6 comments:

  1. Josephine

    Hongera sana kwa hili....kwani kwa muda mrefu inaonekana kulikuwa na nafasi ktk jamii ya blog ambayo ilikuwa haijajazwa. Kweli umekuwa mmbunifu na kwa kuzingatia hali ya kiuchumi ya Watanzania tulio........

    Natanguliza shukrani zangu binafsi na nakuomba kitu kimoja....udhibiti wa matusi na kebehi tu.

    ReplyDelete
  2. inaonekana ni nzuri kwa maana ya mwanzo hivyo ni jukumu la wadau wote waliojiunga na mtandao huu kuboresha na kukuhakisha libeneke linaendelea vizuri na kukua zaidi kwa maana ya kupanuka siku hadi siku.

    Hongera kwa kuanzisha.

    ReplyDelete
  3. WHAT JUST A GOOD PIECE OF WORK YOU ARE DOING! KEEP IT UP AND ROLLING. HONGERA SANA KWA MAONO YAKO YA SAWASAWA NA YA JUU. LABDA NIONGEZE TENA KAMA IFUATAVYO, MARA WATU WANAPOTOA MATANGAZO YAO KWAKO/HUMU NA WAKAFANIKIWA KUPATA WAUME, WAKE AU WACHUMBA NA MARAFIKI NA PENGINE WAKAFUNGA NDOA AU KUTEMBELEANA WARUDI TENA KWAKO NA PICHA WATU WAZIONE KAMA TESTIMONIALS/USHAHIDI ILI IWE MARKETING TOOL IVUTIE WENGINE KUTUMA MAOMBI KUPITIA HUMU NI HILO TU DADA MPENDWA

    ReplyDelete
  4. hi wanablog,
    naamini blog hii pamoja na watumiaji wake hatuko kwenye mizaha,but i can see people starting attaching picha za uchi, we are not after that,let us behave as grown ups! Dada jose, do not entertain these types of people who do not know what they want!

    MDAU.

    ReplyDelete
  5. ni mala yangu ya kwanza kujiunga na mtandao huu, nashukuru sana mdau kwa kutoa onyo kwa wale wanaojirahisisha kuonyesha viungo nyeti kwenye mtandao sio inshu, viungo nyeti huonyeshwa katika sehemu nyeti, tupo kwaajiri ya furaha, kutafutana, kupeana maoni, malengo, pongezi, pole na matumani, hii sio web ya ngono, ikikushinda tuachie wenye shida, binafsi sijaipenda hio ila nachukulia poa tu.

    ReplyDelete
  6. kama kweli kuna mtu kafanya hivyo basi ita kuwa huyo hana heshima,kwani kama kweli wewe ni mtu mwenye akilizako binafsi unajua kabisa kuwa watu wanao ingia huku ni wenye shida mahalum basi,tuwacheni na shida zetu msituharibie wengine jamani kwani hiyo ni tabia mbaya sana sija penda kabisa.

    ReplyDelete